Raila Amefanya Mengi Mlima Kenya Ikilinganishwa na Ruto, Herman Manyora

July 2024 · 2 minute read

Mchanganuzi wa kisiasa Herman Manyora amesema Naibu wa Rais William Ruto amefanya machache mno katika eneo la Mlima Kenya hata wakati anatafuta kura za wenyeji.

Manyora alidai kwamba ingawa Naibu Rais William Ruto kwa sasa anafurahia kuwa na wafuasi wengi katika jamii za GEMA, hawezi kulinganishwa na kinara wa ODM Raila Odinga.

"Huwezi kulinganisha kile Jaramogi alifanya Mlima Kenya na kile Ruto amefanya, huwezi kulinganisha kile Raila amefanya Mlima Kenya, haswa na Kibaki, na kile Ruto amefanya," aliiambia TV 47.

Mchambuzi huyo alikadiria kuwa ni kura ya Mlima Kenya ambayo itakuwa na uamuzi muhimu wa nani atakuwa rais 2022

Pia soma

"Kieleweke Fanyeni Bidii Kumtafutia Raila Kura Mt Kenya, Saa Hii Hana Kura Huko": SK Macharia

"Uchaguzi wa 2022 utaamuliwa juu ya Mlima Kenya. Kwamba ni nani atakayekuwa rais yatakuwa ni maamuzi ya Mlima Kenya. Ni swala la idadi ya wapiga kura. Ruto anahitaji Mlima Kenya kwa hivyo ikiwa kitu kitatokea katika Mlima Kenya na anashikilia uongozi wake na kwamba kuna kitu kinachosababisha asipate asilimia 40 ya kura ya Mlima Kenya, atakuwa ameisha," akaongeza.

Hata hivyo, mbunge wa Mathira Rigathi Gachagua alitofautiana na Manyora akisema mtu yeyote yuko huru kufanya kampeni katika Mlima Kenya

"Sisi ni watu wa kidemokrasia. Raila Odinga anakuja katika mkoa wetu, ana haki ya kidemokrasia, mwacheni aje… lakini William Ruto amekuwa nasi kwa miaka tisa iliyopita. Tuko wengi zaidi ya 40 ambao tunataka kujiunga na UDA. Mimi, Moses Kuria, Martha Karua na Mwangi Kiunjuri tunamtaka William Ruto awe rais," alisema.

Mbunge wa Kandara Alice Wahome hivi karibuni alidai Raila hatakubalika kamwe katika eneo la Mlima Kenya.

"Niliona watu walikuwa wakijifanya eti Raila Odinga anakubalika katika Mlima Kenya kama mgombea wa urais. Kama rafiki, tunamkaribisha Mkenya yeyote yule katika mkoa wetu."

Pia soma

Itakuwa Ngumu Kumuuza Raila Mt Kenya, Kieleweke Wamwambia Uhuru

"Ingawa Raila ni kiongozi katika taifa hili, asidanganyike kwamba anaweza kupenya katika eneo la Mlima Kenya kwa urahisi," alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZ4F2fJhmqZqhnJZ6ornEn5insZFiuqa6xqJkpqSZoq5ut8SnsJplmaC2rbXNoJinoaOdxKJ5zZpkq62kpHqpsdGmmKdlnZa7urvRmmWhrJ2h