-Watu wawili wamejeruhiwa kwenye mlipuko wa kilipuzi cha kujitengenezea Nairobi
- Wawili hao ni msukuma rukwama na muuzaji wa gazeti
-Hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo
Kulingana na walioshuhudia, kifaa hicho kimelipuka katitika makutano ya barabara ya Latema na Tom Mboya eneo la Odeon.
Habari Nyingine : Shambulio la 14 Riverside: Shirika la Msalaba Mwekundu lasema watu 50 bado hawajulikani waliko

Watu wawili wameripotiwa kuumia kufuatia mlipo huo uliotokea muda mfupi baada saa moja jioni, na maafisa wa usalama na wale wa Msalaba Mwekundu tayari wapo katika eneo tukio.
Kulingana na kamanda wa polisi Nairobi Philip Ndolo aliyethibitisha tukio hilo, mlipuko huo ulitokea katika mizigo iliyokuwa ikisafirishwa na mhudumu wa troli.
Ndolo alisema kwamba mtu huyo alikuwa akisafirisha katoni lililokuwa limefungwa kabisa na huenda kulikuwamo vilipuzi.
Ndolo alisema mwanaume mwenye asili ya Kisomali alimwambia msukuma rukwama kwa jina Joseph Okinyi kumbebea mizigo yake na kisha baadaye kujifanya alikuwa amesahau kitambulisho chake.
“ Alimwambia alikuwa amesahau kitambulisho chake na kujifanya kukiendea..aidha, muuzaji wa gazeti aliumia kwenye mguu wake wa kushoto,” alisema Ndolo
Habari Nyingine : Mjukuu wa rais mstaafu Mwai Kibaki, Sean Andrew, afichua jinsi alivyotaka kujitoa uhai
Wakati huohuo polisi wamewataka wananchi kujiepusha na kuingia eneo la tukio kwa kuwa eneo hilo ni la uhalifu ambalo sasa limo mikononi mwa polisi.
Mlipuko huu unajiri wiki moja baada ya uvamizi wa magaidi katika Hoteli ya DusitD2 eneo la 14 Riverside Drive, uliosababisha vifo vya watu 21 na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Habari Nyingine : Uvamizi wa DusitD2: Marafiki wa dhati waliouwawa wakila hotelini wazikwa
Kufikia sasa watu kadhaa wametiwa mbaroni huku uchunguzi wa polisi ukiende;ea kuhusiana na shambulio hilo la kigaidi.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiboRxgpVmrpqspWJ%2FbsPAo5yrrZiexKJ5yrCcp7GVYrqttc%2Buoqhlnpa2s7vBomWhrJ2h