- Munene aliripotiwa kutoweka baada ya dadake kutoweza kumpata kwa simu
- Majirani zake walikiri kuwa hawakuwa wamemuona kwa muda
Wiki mbili baada ya mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Nairobi kuripotiwa kupotea, mwili wake ulipatikana katika hifadhi ya hospitali kuu ya kaunti ya Mombasa, CPGH.
Habari Nyingine: Mwanamume ampa talaka mkewe dakika 15 baada ya kufunga ndoa na kushtua
Mwili wa Dennis Munene, 25 aliyeripotiwa kupotea siku ya Jumatano, Mei 9 ulitambuliwa na familia yake siku ya Alhamisi, Mei 24 katika hifadhi ya maiti ya Coast General Hospital Mombasa.
Tuma neno 'NEWS' kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Habari Nyingine: Barua ya mapenzi ya mwanafunzi wa shule ya upili kwa mwalimu wake yasisimua wengi
Kwa mujibu wa ripoti za Daily Nation, dadake Munene, Mercy Gichangi alisema kuwa alianza kumtafuta nduguye baada ya kukosa kuchukua simu kwa muda.
Aliamua kwenda kumuona kwa nyumba yake mtaa wa Alsops Kasarani siku ya Jumamosi, Mei 12, ila majirani wakamwambia kuwa hawakuwa wamemuona tangu wiki iliyotangulia.
Habari Nyingine: Wanaume wenye wanawake wanene huishi maisha marefu, yenye furaha - utafiti
Ni kuanzia wakati huo ndipo aliporipoti kwa polisi na mpango wa kumsaka ukaanza.
Maafisa wa polisi walianza kuchunguza simu yake Munene huku familia ikimtafuta katika mahospitali na hifadhi za maiti.
Waliambiwa na maafisa wa polisi kuwa simu yake Munene ilitumika mara ya mwisho Jumatatu, Jumatano, Mei 9.
Habari Nyingine: Miguna Miguna afichua jambo lisilo la kawaida kumhusu Raila, adai alikuwa mlevi
"Hatukumpata lakini mnamo Jumatatu, Mei 14 maafisa wa polisi walituambia kuwa simu yake ilitumika mara ya mwisho Jumatao, Mei 9 kabla ya kuzimwa," Alisema.
Walisafiri hadi Mombasa walipoupata mwili wake baada ya mhudumu kukiri kuuona mwili kama walivyomueleza.

Habari Nyingine: Shabiki wa Akothee akipatapata baada ya kuuliza kuhusu chupi yake
Kulingana na ripoti za hifadhi hiyo, mwili wake Munene uliletwa hapo siku ya Jumamosi, Mei 12.
Mwili wake unasemekana kupatikana katika ufuo wa bahari Hindi, Marina Beach eneo la Mtwapa baada ya mwanakijiji kuripoti kwa polisi kuwa aliuona ukielea kwa maji kwa muda wa siku mbili au tatu.
Familia yake Munene ingali na maswali kuhusu tukio la Munene kufa maji.
Read ENGLISH VERSION
Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke , kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibIF6gZdmmZqZlJZ6uq2MrKCkrV2grqW0wGaxmmWbqrq1rcWuq5plnayur63OZp2apZmhtqJ52JqkqZmklnquu8ybmKyZXaCutbXKmmScoKWir6J5wqGYZqOlnbanrcOhoJplnZa2tbWNoaumpA%3D%3D